Lifestyle

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

SIL

Mapenzi kinyume na maumbile chanzo cha ndoa kuvurugika

NDOA AGOMA.jpeg Mapenzi kinyume na maumbile chanzo cha ndoa kuvurugika

Tue, 6 Sep 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Afisa Ustawi wa Jamii wa Jiji la Dar es Salaam, Joyce Maketa, amesema kwamba miongoni mwa mambo yanayovuruga ndoa hadi kupelekea wanandoa kuachana inasababishwa na wanaume kuomba mahusiano kinyume na maumbile.

Kauli hiyo ameitoa hii leo Septemba 6, 2022, jijini Dar es Salaam, kwenye kipindi cha SupaBreakfast ya East Africa Radio mara baada ya taarifa kuonesha kwamba kila mwezi ndani ya jiji la Dar es Salaam takribani ndoa 300 zinavunjika.

"Kumekuwa na mahusiano mapya (Kwa wanandoa) yanayopelekea wakati mwingine kuomba kuwa na mahusiano kinyume na maumbile hicho kimekuwa ni moja ya kitu ambacho kimekuwa kikivuruga ndoa nyingi na watu mwisho kuachana, tuachane na hizo tabia tunazozi-copy na tuishi maisha yanayompendeza Mungu," amesema Joyce.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live