Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mapema tu, Simba yajaza Uwanja

Jaza Pic Data Mapema tu, Simba yajaza Uwanja

Sun, 19 Sep 2021 Chanzo: www.mwanaspoti.co.tz

MASHABIKI wa Simba wameonesha mapenzi ya dhati kwa timu yao baada ya kufika uwanjani leo kwenye tamasha la Simba Day na kuujaza Uwanja  wa Benjamin Mkapa mapema.

Hadi kufika saa 8:15 mchana tayari majukwaa yote ya uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua watu 60,000 yalikuwa yamejaa mashabiki waliovalia jezi za Simba kwa wingi.

Sambamba na kujaza Uwanja, pia tiketi zote za kuingia uwanjani hapo leo zimeuzwa na kuisha kabla ya saa nane mchana kwa mujibu wa klabu hiyo.

Hata hivyo nje ya uwanja huo bado kuna nyomi la watu ambao wamepanga foleni kwenye mageti wakisubiri kuingia ndani huku wengine wakiburudika kwa aina tofauti.

Chanzo: www.mwanaspoti.co.tz