Menu ›
Burudani
Fri, 17 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Haji Manara ameibua gumzo la aina yake baada ya kuonekana 'very close' na mtoto wa mjini Zaylisa usiku wa kuamkia leo Novemba 17, 2023 pale Super Dome, Masaki jijini Dar.
Kwenye halfa hiyo ya kumtambulisha msanii mpya wa Wasafi Classic Baby (WCB), D Voice, Manara alionekana beneti na mrembo huyo ambaye aliolewa na kuachwa na msanii wa Singeli, Dulla Makabila.
Walikaa pamoja na kuna wakati, Manara alionekana akicheza naye muziki kwa ile staili ya 'bibi mbele, bwana nyuma' huku wakishikana kimahaba.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live