Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mama asimulia alivyowakuta mtoto wake na mume wake kitandani

75c5ec386848afaa Mama asimulia alivyowakuta mtoto wake na mume wake kitandani

Tue, 26 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mary, ambaye ni mpangishaji mtaani Kangemi, Nairobi amekata tamaa kupenda baada ya mpenzi wake mwenye umri wa miaka 32, kutoweka na binti yake. Mama huyo mwenye umri wa miaka 55, alimkaribisha Odhis nyumbani kwake wiki mbili baada yao kukutana na walichumbiana kwa miaka minne kabla yake kumsaliti.

Siku moja aliporejea nyumbani jioni akitokea mazishini, Mary, alimfumania Odhis na binti yake wakishiriki ngono kwenye kitanda chake lakini bila kujali waliendelea na walichokuwa wakifanya Mary alisema anajutia kumpenda mwanamume mchanga kumliko akiwashauri wanawake kuwa waangalifu wakati wanawalika wageni nyumbani kwao.

Akizungumza na TUKO.co.ke, mama huyo mwenye umri wa miaka 55, alisema alimpoteza mume wake miaka saba iliyopita, na miaka miwili baadaye alikutana na mwanamume kwa jina Odhis.

"Alikuwa akiishi katika ploti yangu na sijawahi kumuona na mwanamke. Tukawa karibu na baada ya wiki mbili, alikuwa amehamia kwenye nyumba yangu ambayo nilikuwa naishi na mtoto wangu wa pekee wa kike," alikumbuka.

Mary alisema alikosolewa kwa kuchumbiana na mwanamume ambaye anatosha kuwa mwanawe lakini aliwapuuza mahasidi na kujishughulisha na mpenzi wake mpya.

Wawili hao walichumbiana kwa miaka minne na uhusiano wao ulionekana kuwa sawa bila doa.

"Alinifanya nipende tena. Alikuwa akinifanyia kazi za nyumbani, yaani, kunipikia, kunifanyia usafi wa nyumba na kila jioni alikuwa akinifanyia massage ya kina kirefu. Ndani ya miaka minne, niliweza kumuamini na hata kumpa nambari zangu za siri za akaunti yangu ya benki. Ningemtuma atoe pesa na kuninunulia vifaa vya ujenzi na hakuwahi kuiba hata senti moja," Mary alisumulia.

"Hata nilinunua kipande cha ardhi huko Kasarani na kumjengea nyumba, ambapo tungeishi miaka yetu ya mwisho duniani," aliongezea.

Apata pigo kubwaMary alisema siku moja alirejea nyumbani akitokea mazishi eneo la Maragua, na mvua kubwa ulikuwa unanyesha.

Aliingia katika nyumba lakini hakumpata yeyote sebuleni ilhali runinga ilikuwa imewashwa na kuwekwa sauti ya juu.

"Nilienda jikoni na Odhis hakuwepo. Kwa hivyo nilifikiri anapika mandazi nilikuwa nimemwomba aandae kwa sababu nilikuwa nimemwambia ningefika asubuhi iliyofuata na jamaa wachache," alisimulia.

AwafumaniaLakini mpenzi wake hakuwepo, mama huyo alidhania kuwa huenda alikwenda dukani na binti yake alikuwa amewatembelea marafiki zake.

“Niliamua kwenda kwenye chumba changu cha kulala ambacho kiko ghorofani ili nibadilishe nguo lakini wakati nikipanda ngazi nilipokelewa na sauti zisizo za kawaida, mtu alikuwa akilalama kwa nguvu na kadri nilivyopanda ngazi ndivyo zilivyozidi kusikika."

"Nilifikiri Odhis alikuwa akitazama video za watu wazima kama tulivyozoea tukiwa chumbani," alisimulia.

Hakudhania kuwa mpenzi wake alikuwa akirusha roho na mtu mwingine.

“Nilipofika mlangoni ulikuwa wazi na taa zimewashwa, Odhis na binti yangu wakila uroda kwenye kitanda changu, nilishtuka lakini tena ilibidi niwe na nguvu, nilisubiri kwa dakika 30 kisha nikaingia ndani," alikumbuka.

Licha ya kumuona Mary, wawili hao bila kujali waliendelea na walichokuwa wakifanya.

"Nilimpiga binti yangu kofi kali sana na akanirudishia kofi. Nilishtuka jinsi mambo kama hayo yanaweza kutokea duniani. Wawili hao walichukua nguo zao, wakashuka chini, wakiniacha nikiwa nimesimama," alisimulia.

Mary alisema aliwafuata wawili hao lakini tayari walikuwa wameondoka na ni mwaka moja sasa bila yeye kuzungumza na binti yake wala mpenzi wake.

MajutoMary alisema anajutia kumpenda mwanamume mchanga kumliko akiwashauri wanawake kuwa waangalifu wakati wanawalika wageni nyumbani kwao.

"Nilimuahidi mume wangu akiwa karibu na kifo chake kwamba sitawahi kumpenda mtu mwingine lakini kwa sababu niliumia moyoni, niliona ni sawa kuendelea ili kusahau hasara yake lakini baadaye niligundua kuwa nilifanya makosa," alisema.

"Nimemsamehe binti yangu, na ningetamani kukutana naye siku moja. Lakini kwa Odhi, sitaki kumuona tena. Aliharibu maisha yangu na kumchukua binti yangu," aliongeza.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke