Mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 19 nchini Brazil, amejifungua mapacha wawili wenye baba tofauti.
Baada ya kujifungua watoto hao, mama huyo alipewa majibu ya DNA na mchumba wake na kuambiwa kuwa mtoto mmoja tu ndiyo alikuwa wa mwanaume huyo.
Aidha, baada ya kufahamu hilo, mwanamke huyo alifunguka na kusema kuwa alishiriki tendo la ndoa na wanaume wawili tofauti kwa siku moja hivyo hakujua kama inawezekana kupata watoto kwa baba tofauti.
Madaktari na wataalamu walifafanua jambo hilo lililowashangaza wengi, kuwa inawezekana kwa mayai mawili ya mama mmoja kurutubishwa na mayai ya baba wawili tofauti huku watoto hao wakikuwa kwa kutumia mifuko ya uzazi tofauti tumboni kwa mama yao.
Je, kwa upande wako unadhani jambo hili linawezekana? Dondosha comment yako hapo chini.