Mama Mzazi wa Mwanamke aliyefariki dunia siku ya harusi afungua mashitaka ya kudai urithi wa mali za mtoto wake aliyefariki dunia siku ya harusi
Mwanamke huyo aliyetambulika kwa jina la Lisa Miller ameibuka kudai mali alizochuma mtoto wake huyo wa kike enzi za uhai wake. Mtoto wake aitwaye Samantha Miller alifariki kwa kugongwa na gari siku ya harusi yake na mume wake Aric Hutchinson huko nchini Marekani.
Miezi kadhaa toka kutokea kwa tukio hilo mwanamama huyo amefungua mashitaka ya kudai mali za mtoto wake ambaye anadai kuwa mtoto wake huyo kama angekuwa hai basi angempa mali zake zote . Samantha ameacha mali nyingi ikiwemo nyumba za kifahari ambazo alizichuma kabla ya kuolewa na mwanaume huyo.