Menu ›
Burudani
Fri, 29 Sep 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mama Mzazi wa muigizaji Wema Sepetu usiku wa jana kwenye birthday ya mtoto wake ametema nyongo kwa kuwachana Whozu na Wema kuwa hapendezwi na maisha yao ya kuishi bila kujirasimisha kwa wazazi.
Mama Wema anasema kuwa wanawadhalilisha wazazi kwa kitendo cha wao kuishi bila kuweka taratibu sawa kwa maana wazazi wa pande zote mbili wajue ndoa na mahusiano yao.
"Mimi leo hapa nimekuja na kaka yangu yupo pale, ananiambia dada tutoke. Nataka mtuheshimu sisi wazazi," alisema mama Wema.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live