Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mama Diamond kafunguka ni kuhusu Diamond na Zari

151 Screen Shot 2017 12 13 At 7.41.30 PM 660x400.png TZW

Fri, 15 Dec 2017 Chanzo: millardayo.com

Leo December 13, 2017 kupitia ukurasa wa instagram wa mama yake na muimbaji wa Bongofleva Diamond “Sandrah” ameamua kuandika ya moyoni kuhusiana na kile ambacho huwa anapost kwenye page yake ya instagramna watu kuanza kutoa comment tofauti tofauti huku wengine wakikosoa.

Mama Diamond mara nyingi katika ukurasa wake wa instagra hupost kazi za mwanae za  kisanaa na wakati mwingine anampost mtoto wake Diamond Platnumz na mpenzi wake Zari the Boss Lady, hivyo huwa haishangazi kuona akiwapost wawili hao ila caption ya leo kwenye picha aliyowapost Diamond na Zari imechukua headlines.

Ujumbe wa mama Diamond katika post yake ya instagram haujaweka wazi ni nini kimemfanya aandike maneno kama hayo katika picha aliyowapost Diamond na Zari lakini baadhi ya watu wanautafsiri ujumbe huo kama onyo kwa mtu, au shabiki anayecomment vitu visivyompendeza baada ya kuwapost Diamond na Zari.

 

Kupitia picha hiyo aliyoipost leo December 13,2017 katika ukurasa wake instagram ameandika caption inayosomeka

“Mapenzi niliyonayo kwa wanangu hawa hayana mfano…Ninapompost mkwe wangu @zarithebosslady au mwanangu @diamondplatnumz sifanyi kwa ajili ya kuwaridhisha WASIOTUPENDA….Nawapost kwa mapenzi makubwa kwao na wajukuu zangu @princess_tiffah @princenillan Imani yangu si kumkwaza mtu au kumkebehi mtu bali Nawapendaaa sana…Akaunti hii ni MALI yangu hivyo asitokee MTU kunipangia cha kupost au kujifanya Mama/Baba ushauri… Maisha ni kuchagua na si kuchaguliwa #StrongFamily#TusipangianeChaKupost#NajitambuaKulikoMjuavyo#ABoyFromTanda“

MOBETTO:” Yani naskia bila mimi huwezi kabisa Mrs Fudenge

Chanzo: millardayo.com