Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mabeste afikishwa polisi na mzazi mwenziye

MABESTE Mabeste afikishwa polisi na mzazi mwenziye

Tue, 2 Jun 2020 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Msanii Mabeste ameteka vichwa vya habari vya burudani siku ya leo Juni 1, 2020, baada ya kuitwa kituo cha Polisi Oyster Bay kwa kosa la kumchafua mitandaoni mzazi mwenziye na mkewe wa zamani Lissa.

Akizungumza na EATV & EA Radio Digital, Mabeste amesema ameenda kituo cha Polisi na anasubiria hadi atakapopangiwa kwenda tena na kosa ni kumchafua kupitia wimbo wake mpya wa Back Off na kumtangazia kwa watu na kwenye vyombo vya habari kwamba mtoto aliyekuwa naye sasa hivi ni wake.

"Ishu ni kwamba nilikuwa nimeshtakiwa na mzazi mwenzangu kwamba namdhalilisha, nimeenda kusikiliza malalamiko yake ambayo anadai kwamba nimemchafua kwenye mitandao kupitia wimbo wa Back off, kuwa unamlenga yeye katika kumdhalilisha zaidi, kingine ni mtoto wake aliyempata sasa hivi, anadai natangaza kwamba ni wa kwangu kwa hiyo inamletea shida kwenye mahusiano yake" amesema Mabeste.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live