Menu ›
Burudani
Thu, 24 May 2018
Chanzo: bongo5.com
/>
Mwaka jana Kizz Daniel alikiuka masharti ya mkataba wake na G-World Ent. kwa kutangaza kufungua lebo yake ya Flyboy Inc, jambo ambalo lilipelekea uongozi wa G-World Entertainment kumfungulia mashtaka Kizz Daniel.
Mwanzoni mwa mwezi Januari mwaka huu Mahakama mjini Lagos ilimpiga marufuku msanii huyo ku-perfom nyimbo zake zote alizotoa kipindi yupo chini ya lebo hiyo au kutumia jina lake kibiashara mpaka kesi itakapomalizika.
Kwa sasa Kizz Daniel tayari ameshabadilisha jina lake lililozoeleka la Kiss Daniel kwenye platform zote za muziki na kurasa zake za mitandao ya kijamii kama mahakama ilivyoamuru.
“Walk away from anything that gives you bad vibes. You don’t have to make sense of it or make clear. It’s ur life, do what makes you happy ”
Chanzo: bongo5.com