Safina Namukwaya, mwanamke mwenye umri wa miaka 70, mkazi wa Wilaya ya Masaka, amewashangaza watu wengi baada ya kujifungua watoto mapacha katika hospitali moja huko nchini Uganda.
Safina Namukwaya, mwanamke mwenye umri wa miaka 70, mkazi wa Wilaya ya Masaka, amewashangaza watu wengi baada ya kujifungua watoto mapacha katika hospitali moja huko nchini Uganda. Bi Safina amejifungua mvulana na msichana mmoja akiwa na uzito wa kilo 1.7 kila mmoja katika Kituo cha Kimataifa cha Upandikizaji, cha Hospitali ya Wanawake mjini Kampala, ambako alikuwa amekaa kwa siku tano kwa maandalizi ya kujifungua katika chumba cha faragha.