Menu ›
Burudani
Thu, 12 Nov 2020
Chanzo: zanzibar24.co.tz
Mwanamziki mkongwe wa bendi ya Talent nchini Tanzania, Hussein Jumbe katika hali isiyo ya kawaida amepata ajali akiwa amelala (ndotoni) na kuvunja Mguu wake wa Kulia .
Mzee Jumbe ambae aliwahi kutamba na wimbo wake wa “Nachechemea” uliojizolea umaarufu Mkubwa sana, anasema kuwa hadhani kuwa ndoto hiyo ni ya kawaida Ila yote anamuachia Mungu .
Msanii huyo alisema kuwa aliota anakimbizwa na kuku na kujikuta akimpiga mateke, kumbe alikua anapiga Ukuta kitu kilichompelekea kuvunja Mguu wake wa kulia .
Chanzo: zanzibar24.co.tz