By Kelvin KagamboMore by this Author KATIKA toleo lililopita tuliona maisha ya Mkojani kabla hajawa maarufu. Ambapo alifuchua alikuwa ni mchekeshaji wa mtaani wa kuweka tumbo kubwa na kujipaka masizi usoni. Pia alielezea kuwa alikuwa kwenye Ze Komedi ya kwanza ya kina Joti na Mpoki kabla hawajamtoa kwenye kundi hilo bila kumpatia sababu za msingi.
Leo anaongelea maisha yake ya umaarufu yalipoanza.
KILICHOMPA
USUPASTAA
Mkojani anakwambia licha ya kwamba alianza kuigiza muda mrefu, tangu mwaka 2008 alipotoa filamu yake ya kuitwa Kigodoro, lakini umaarufu aliupata miaka ya hivi karibuni baada ya kuigiza kama Mkojani.