Muigizaji Lupita nyongo athibitisha kuachana na mpenzi wake Selema.
Lupita ametumia ukurasa wake wa Instagram kuelezea maumivu makali anayopitia kwa sasa. Ameandika;
"Nimechoka kuliweka hili moyoni na kuuficha ukweli unaoniumiza. Ni muhimu kuweka wazi kuliko kukaa kimya na kuacha nikihusishwa na mtu ambaye siwezi kumuamini tena. Nakubaliana na hali ninayoipitia sasa kwani najua maumivu ninayo yapitia ni sawa na upendo nilionao."
Lupita anaendelea kwa kuandika;
"Nimeweka wazi hili ili iwe fundisho kwa wengine wote wanaopitia mazingira ya kuumizwa kimapenzi kama mimi."
Lupita na Selama waliweka wazi mahusiano yao mwishoni mwa mwaka 2022.