Lifestyle

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

SIL

Lulu Hassan kuwazawadi watoto waliomuiga na mumewe mtindo wao wa utangazaji

984835d82f759641 Lulu Hassan kuwazawadi watoto waliomuiga na mumewe mtindo wao wa utangazaji

Wed, 5 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Watoto wabunifu kutoka kundi la Hurumatown kwa mara nyingine wamewachangamsha wafuasi wao baada ya kuiga tangazo la kumkaribisha Rashid Abdalla na Lulu Hassan kwenye Citizen TV

- Watoto hao waliiga namna Abdalla na Lulu huangaliana na jinsi Bi Mswafari huongea na kuvalia wakati wa mahojiano

- Mashabiki wa Lulu walimuomba awasake watoto na kuwaleta studioni wakati wa shoo ya Nipashe

Mwanahabari wa runinga Lulu Hassan ameelezea namna alifurahishwa na watoto wa Hurumatown ambao waliigiza tangazo la Citizen TV wakati alikuwa anamkaribisha mume wake Rashid Abdalla kujiunga na kituo hicho.

Watoto hao ni maarufu kwa kuwaiga wanahabari na ubunifu wao umewasaidia kupendwa zaidi na watu hao tajika.

Huku wakiiga tangazo hilo la Citizen TV, watoto hao wanaonyeshwa wakiendesha gari la kujitengenezea kama Lulu alivyofanya.

Kutokea kwa uchongezi wa maneno ya mnato na namna watangazaji hao maarufu huangaliana, ama kweli waliwaiga kwa ufasaha.

Hiki ndio kile Lulu aliandika kwenye Instagram: "@hurumatown80 sisemi kitu. Tumenyenyekea na tunajivunia nyinyi nyote. Zawadi zinakuja"



Hii hapa maoni ya wafuasi:@ynscollections2: "Wana talanta naomba wapate hizo zawadi."

@pauynnegrete alisema: "Weeeh tafadhali watafute Lulu, ni moto."

@idris.shamim: "Ni wabunifu sana."

@__fatma_muhiddeen_kayla__ : "Wow, mashallah, huu ni ubunifu wa kipekee."

@iamsarrywamz alisema:' "Hii iko sawa! Walete Nipashe Wikendi siku moja."

@just_polyne commented: "Ubunifu wao ni sawa tu."

Watoto hao wa Hurumatown hivi majuzi waliangaziwa na TUKO.co.ke baada ya kumuiga mwandishi wa habari wa shirika la BBC Larry Madowo.

Madowo alipakia video ya watoto hao wawili wakiiga tukio ambapo mwavuli wake ulijaribu kumtatiza akiwa hewani.

Mtoto mmoja alikuwa anaiga maneno ya mwanahabari huyo huku mwingine akifuatilia ishara za Madowo.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke