MWANAMUZIKI wa kizazi kipya, Linex Sunday, amesema tayari ameachia albamu yake fupi ‘EP’ ambayo inaitwa Dunia Nyingine ikiwa na nyimbo sita.
Akizungumzia albamu hiyo, alisema tayari ameshatoa baadhi ya nyimbo kutoka katika albamu hiyo ikiwemo Dunia Nyingine, huku akisubiri muda atoe nyimbo nyingine.
Alisema miongoni mwa wasanii ambao amewashirikisha katika kuikamilisha albamu hiyo ni Mimi Mirs mdogo wake na Vanesa Mdee pamoja na mwanamuziki Gemma.
“Ni mbivu au mbichi nisaidie kuwajuza na wale kwa kushiriki na marafiki zako nami nitashukuru,” alisema.
Linex alifanya vizuri na wimbo wa Salima, akiwa na mwanamuziki Nassib Abdul ‘Diamond Platnumz’ lakini baadaye alipotea kabla ya kuamua kurudi tena kwa nguvu.