Menu ›
Burudani
Thu, 7 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwanamuziki mkongwe wa Bongo Fleva nchini Lady Jaydee amewataka walimu kutumia nyimbo zake kufundishia shuleni.
Ameyasema hayo kupitia Instagram yake baada ya 'kuposti' video ikionesha polisi akiongea na wanafunzi kuhusu maisha yao ya sasa na baada ya shule na kuwatolea mfano wa moja kati ya wimbo wa mwanamuziki huyu ‘Historia’ uliotoka miaka mitatu iliyopita.
Komando Jaydee ameandika;
“Jamani tumieni nyimbo za Ledi Jeidiii kufundishia watoto mashuleni, au hadi Marekani waanze?”
Chanzo: www.tanzaniaweb.live