Ikiwa leo ni siku ya beer Duniani ijue hii rekodi, achana na mnywaji Piere Liquid wa Tanzania , huko nchini Ufaransa Kuna Mwamba Anaitwa Andre The Giant , mcheza mieleka mstaafu ambae anafahamika zaidi kwa rekodi zake za kunywa bia Kama vile anakunywa maji.
Andre ambae ni jitu la miraba minne , alikua hawezi kusafiri kabla ya kulewa, na kwa kawaida alipenda kusafiri na 'kreti' 10 mpaka 14 za bia.
Andre alikua na uwezo wa kunywa bia 108 ndani ya dakika 45 TU!! Kitu ambacho si cha kawaida, na kwa Mujibu ya Daily Telegraph jamaa huyu alikua anapiga jumla ya bia 148 kwa mkao mmoja .
Watu wengi wanaopenda pombe Kali watakwambia Vodka Ni moja na vinywaji vigumu kunywa, lakini Andre alikua na uwezo wa kunywa chupa 40 za Vodka Kama anakunywa juice
Je, unahisi kuna mtu wa Kufikia uwezo wa Mwamba huyu ikiwa Leo ni siku ya bia Duniani ?