Menu ›
Burudani
Mon, 3 Jan 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
SUPASTAA wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz amemmnunulia bonge la zawadi mama yake mzazi, Bi Sanura Kassim aka Sandra ama Mama Dangote kwa ajili ya kuufungua mwaka mpya 2022.
Kupitia insta story ya Mama Dangote, ameandika maneno ya kumshukuru mtoto wake kwa kumzawadia zawadi ya cheni yenye thamani ya zaidi ya Dola za Kimarekani 48,000, sawa na Tsh milioni 110.688.
“Kuzaa kuzuri, Asante baba wangu Naseeb Kichwa @diamondplatnumz 48,000$” anaandika @mama_dangote.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live