Lifestyle

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

SIL

Kibaka abakwa na mwanamke alietaka kumuibia kwa siku 3

FNgP4JxX0AYZwrR Kibaka abakwa na mwanamke alietaka kumuibia kwa siku 3

Wed, 7 Feb 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Wanasema ishi uyaone...Dunia haiishiwi vituko.

Tukirudisha historia nyuma kidogo, mwaka 2011 kibaka mmoja huko nchini Urusi aliyefahamika kwa jina Viktor Jasinski alivamia saluni ya kike inayomilikiwa na mwanamke aliyefahamika kwa jina la Olga Zajac ambaye ni mcheza karate.

Lengo la uvamizi kwenye saluni hiyo lilikuwa ni kuiba chochote kitakachomfaa lakini kwa bahati mbaya akakutana na kipande cha dada tena mbabe kweli kweli.

Inasemekana kuwa dada huyo alimzidi nguvu kibaka na akamkamata kisha kumfungia ndani kwa siku tatu huku akifanya naye mapenzi kwa lazima (akimbaka).

Zolga alikuwa anafanya kazi ya kumlisha dawa za kuongeza nguvu za kiume kisha anamlazimisha wafanye mapenzi. Baada ya siku tatu kupita Zolga alimfungulia kijana huyo na kumruhusu aondoke.

Tukio hilo lilikuja kufahamika baada ya kijana huo kwenda kutoa taarifa polisi kuwa amebakwa na Zolga. Polisi waliamua kuwatia nguvuni wote wawili, kibaka na mbakaji!

Picha linaanza Polisi walipofika kumhoji mwanadada Zahjac na haya ndiyo aliyoyasema....."Mwanaharamu huyo. Ndiyo, tulifanya mapenzi mara kadhaa. Lakini nilimnunulia jeans mpya, nikampa chakula na hata kumpa hela alipoondoka."

Chanzo: www.tanzaniaweb.live