Rapa maarufu kutoka nchini kenya, Brian Ouko Omollo aka Khaligraph Jones ametoa ushauri kwa wasanii wa Kenya kuwa endapo wanataka kufanikiwa kwenye muziki na kuutaawala kama zamani, lazima waungane kufanya kolabo na kumaliza toafuti zao.
Khaligraph amesema hayo ikiwa ni siku chache baada ya baadhi ya wasanii wa Kenya kukiri kuwa nchi hiyo imeporomoka kimuziki na sasa Tanzania ndiyo kinara wa muziki Afrika Mashariki.
"Naamini kwenye kolabo. Orodha ya wasanii wote Kenya tuwe kwa group moja Kenyan Music inaweza ku-take over, tukifanya hivyo ndani ya miezi miwili tu tunakuwa juu," amesema Khaligraph Jones.
Nini maoni yako kuhusu ujumbe huu wa Khaligraph?