Mbunge wa Viti Maalum Khadija Shaaban Tayamaarufu kama Keysha akichangia makadirio ya mapato na mtumizi ya Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa mwaka wa fedha 2024/25 ameiomba Wizara hiyo kuwafundisha maadili Wasanii wa Tanzania akidai kwa sasa yameharibika.
“Nyimbo zimekuwa na maneno ya ajabu sana nawaambia ya moyoni Babu Tale ni Msimamizi wa karibu wa Wasanii lakini anavyosikiliza hizo nyimbo hawaambii kuwa hazina matamshi mazuri na hapohapo nyumbani kwake hakuna bongofleva inayosikilizwa na Mtoto wake.
"Lakini Watoto wetu huko mtaani ambako hakuna wazazi wa kuwasimamia wanaweza kuharibika kwa sababu ya muziki wanaoutoa sasahivi hauna lugha nzuri wala tafsida nzuri,” amesema Keysha.