Menu ›
Burudani
Wed, 21 Mar 2018
Chanzo: bongo5.com
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo March 21 ime imeisogeza mbele kesi ya mrembo wa video nchini Agnes Gerald maarufu kama Masogange.
Mrembo huyo ambaye anatuhumiwa kwa kesi ya utumiaji wa madawa ya kulevya, imeahirishwa kutokana na wakili wake Ruben Simwanza kudai mteja wake huyo amelazwa katika hospitali moja hapa jijini Dar es salaam.
Hakimu ambaye anasikiliza kesi hiyo, Willbard Mashauri ametaja tarehe nyingine itakayoendelea kesi hiyo ambayo ni April 4 ya mwaka huu.
Chanzo: bongo5.com