Menu ›
Burudani
Wed, 20 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mahakama Kuu Masjala ya Wilaya, Arusha, imeahirisha shauri la msanii wa Bongo Fleva, Marioo na Meneja wake Sweetbert Mwinula, wanaodaiwa zaidi ya TZS milioni 500 kwa kuvunja mkataba, Shauri hilo limesogezwa mbele hadi Mei 6, mwaka huu.
Hii ni kufuatia kutokuwepo Mahakamani kwa Jaji Joachim Tiganga anayesikiliza kesi hiyo.
Marioo alifunguliwa kesi na Kampuni ya Kismaty kwa madai ya kuvunja mkataba wa kutumbuiza kwenye hafla ya Mr & Miss Vyuo Vikuu Kanda ya Kaskazini Septemba 23, 2021.
Hata hivyo, upande wa mdai ulifika Mahakamani hapo licha ya kuwa wadaiwa kutokufika Mahakamani.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live