Menu ›
Burudani
Fri, 8 Oct 2021
Chanzo: eatv.tv
Hitmaker wa Bongo Fleva, Kayumba ameonyesha nia na matamanio ya kutaka kufanya kazi ya pamoja (collabo) na kaka zake kwenye game ambao ni Mwana FA, AY na Ommy Dimpoz.
Kayumba amefunguka hilo kupitia ukurasa wake wa instagram baada ya ku-post picha na wakali hao wa Bongo Fleva walizopiga kwenye siku ya usikilizwaji wa albamu mpya ya Alikiba 'Only One King' na kuambatanisha ujumbe wenye matamanio ya kufanya chorus kwenye wimbo utakaowakutanisha pamoja.
Chanzo: eatv.tv