Msanii wa Bongo Fleva, Kayumba amesema, tetesi za kwamba amesainiwa katika lebo ya Next Level Music zimeibuka kwa sababu ya ukaribu wake na Rayvanny.
Amesema amekuwa akipiga stori kwa ukaribu na hata kufanya kolabo na bosi huyo hivyo itakuwa ndio sababu ya watu kuzungumza kwamba huwenda amesaini Next Level.
“Mimi Rayavanny ni mshkaji tunashirikiana naye kwenye mambo mengi angekuwa anataka nijiunge katika lebo yake angekuwa ameniambia, sisi ni marafiki tu,” alisema Kayumba.
Kayumba ni mshindi wa Shindano la Bongo Star Search 2015 na sasa anaendelea kufanya poa kwenye ulimwengu wa Bongo Fleva.