Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kanye West awakosha Wanaigeria na Wakenya

Kanye West Post.jpeg Kanye West awakosha Wanaigeria na Wakenya

Wed, 7 Feb 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mwanamuziki wa mtindo wa rap wa Marekani, Kanye West amewasisimua mashabiki wake nchini Kenya na Nigeria baada ya kuorodhesha nchi hizo mbili miongoni mwa maeneo anayoweza kufanyia tamasha zake mpya.

Orodha fupi ya kumbi ulioshirikiwa kwenye hadithi za Instagram za West inaonyesha kuwa rapa huyo anapanga kutumbuiza katika Eko Energy City mjini Lagos na Uwanja wa Kimataifa wa Nyayo jijini Nairobi.

West pia alielezea nia yake ya kutumbuiza katika Piramidi za Giza za Misri.

Ingawa Kanye West hajatoa tangazo rasmi, orodha hiyo ya safari ya kimuziki imechochea hamu kubwa miongoni mwa mashabiki wa nchi hizo mbili, huku baadhi yao wakishiriki utani kuhusu tamasha hilo kwenye mitandao ya kijamii.

"Kanye hadi Kenya? Labda jamaa alisema lazima atembelee nchi ambayo ina silabi sawa na yeye,"Mkenya mmoja alichapisha kwenye X.

Baadhi ya mashabiki pia walitania kwamba mwanamuziki huyo atangaze bei za tiketi mapema ili waweze kununua.

Mashabiki kutoka nchi kama vile Afrika Kusini wamelalamika kuhusu kuachwa nje ya ziara hiyo, wakirejea wasiwasi kama huo wa siku za nyuma ambao wanamuziki wakuu wa nchi za Magharibi huliondoa bara la Afrika kwenye ratiba zao za utalii wa muziki wa kimataifa.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live