Menu ›
Burudani
Tue, 13 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Unaambiwa rapa Kanye West ‘Ye’ amejawa furaha ya mahusiano/ndoa kwa mke wake Bianca Censori na kila siku kwao ni Valentine's Day mahaba mwanzo mwisho.
West amefunguka hilo baada ya mashabiki kuanza kujaji anavyompost mkewe mitandaoni siku za hivi karibuni akiwajibu kwa kuwaambia ataendelea kumpost sababu ndio furaha yake na anafurahishwa na jambo hilo.
“Nampost mke wangu ninavyotaka, inanifurahisha watu wengine hawataki ufurahi wanataka uwafurahishe. Niliamua kujifurahisha na nimefurahishwa na hilo” amesema Kanye West
Lini mara ya mwisho kupostiwa na mpenzi wako mitandaoni?
Chanzo: www.tanzaniaweb.live