Kane Tanaka mtu aliye na umri mkubwa kupita wote (aliyethibitishwa) ametimiza miaka 119 siku ya jumapili, kwa mujibu wa kitukuu chake Junko Tanaka aliyeposti taarifa hiyo katika mtandao wa twitter.
Kane Tanaka mtu aliye na umri mkubwa kupita wote (aliyethibitishwa) ametimiza miaka 119 siku ya jumapili, kwa mujibu wa kitukuu chake Junko Tanaka aliyeposti taarifa hiyo katika mtandao wa twitter. Bibi huyo alizaliwa mwaka 1903,aliolewa akiwa na umri wa miaka 19 na alifanya kazi kwenye biashara ya familia mpaka alipotimiza umri wa miaka 103. Kitabu cha Guiness kinachoweka rekodi kubwa za kidunia kilimtambua Kane kama mtu mzee kuliko wote mwaka 2019.