Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kama mnaona tumekonda, leteni show tunenepe – Ruby

9943 34643181 2155229344722356 1157828444612984832 N TZW

Mon, 25 Jun 2018 Chanzo: bongo5.com

Msanii wa muziki Bongo, Ruby amefunguka kuhusu stori zinazodai kwa sasa mwili wake umepungua (amekonda) ukilinganisha na hapo awali.



Muimbaji huyo anayetamba na ngoma ‘Niwaze’ ameiambia FNL ya EATV kuwa picha zilizokuwa zikisambaa kwenye mitandao hajui zimetokea wapi.

Ruby alienda mbali zaidi kwa kueleza kuwa picha hizo zimefanyiwa editing na wale wanaoeneza stori hilo wampe kazi (show) ili anenepe.

“Halafu kitu kingine basi wawe wanaleta shows, kazi ili tunenepe, hivyo ndio vitu vya kuongea. Kama mnaona tumekonda, mnataka tunenepe, mnaleta shows, kazi,” amesema Ruby.

Ruby alikuwa kimya kwa kipindi kirefu katika muziki mara baada ya kuzinguana na menejimenti yake ya zamani. Wimbo wa kwanza kutoa kwa mwaka huu ni Niwaze aliowashirikisha kundi la The Mafik.

Loading...
Chanzo: bongo5.com