Menu ›
Burudani
Mon, 8 May 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Muigizaji Kajala Masanja na msanii wa Bongo Fleva, Marioo wanaonekana kuelewana kinyama kufuatia kuonekana wakiwa pamoja na kucheza pamoja.
Kajala ameonekana nyumbani kwa Marioo akicheza kibwagizo cha wimbo mpya wa Marioo uliopo kwenye albamu yake ya The Kid You Know.
Kajala ameonekana akijiachia bila wasi kitovu nje wakidansi na kufurahi pamoja na Marioo.
Ikumbukwe mtoto wa Kajala, Paula kwa sasa ndiyo mpenzi wa Marioo hivyo ni kama mtu na mkwewe wanacheza pamoja.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live