Baada ya msanii wa muziki nchini Tanzania Harmonize kumtambulisha mtoto wake wa nje ya ndoa , kupitia ukurasa wa kijamii wa Instagram wa mke wa msanii huyu bibie Sarah ameandika ujumbe mzito ambao uliwashagaza wengi .
“Mungu wangu watu kweli wamevurugwa, mara mbili wamepima DNA ya mtoto bado majibu ni Negative, ila kwa kuwa umeshindwa kupata mtoto umeamua kujipa mtoto asie wako”
“Hongera kwa adoption, utakua na roho nzuri hukujua jinsi ya kutunza mke sababu ya maovu yako natumai utajua kutunza mtoto, ukome kuongopea mashabiki dah, nimepost hii kwa lugha ya kiswahili kila mtu ataelewa“ aliandika Sarah