Mwimbaji Staa wa Bongofleva juma jux pamoja na Wasaidizi wake wamenusurika katika ajali ya gari iliyotokea leo maeneo ya Nungwi Unguja Zanzibar wakielekea Kendwa Rocks baada ya Gari aina ya Coaster kufeli breki na kukosa mwelekeo kulikosababisha kulifuata gari walilokua wakisafiria ( Range Rover) na kuligonga ubavuni.
Raymond Maziku ambaye ni Meneja wa Jux ameiambia ameeleza kuwa ni Mtu mmoja tu aliyepata mshtuko kwenye ajali hiyo na kuwaishwa Hospitali lakini wengine wote wakiongozwa na Jux wametoka salama na wanaendelea na maandalizi ya show yao itayofanyika Kendwa Rocks Zanzibar Jumamosi ya kesho.
Tazam Video hapa Chini;