Muigizaji wa Marekani, Jussie Smollettt amehukumiwa kifungo cha siku 150 jela baada ya jopo la mahakama kugundua kuwa alidanganya polisi kuwa ameshambuliwa.
Nyota huyo wa zamani wa tamthilia ya Empire, mwenye umri wa miaka 39, alipatikana na hatia mwezi Desemba kwa mashtaka matano ya kufanya fujo baada ya kutoa taarifa za uongo kuhusu shambulio hilo la uwongo.
Adhabu hiyo pia inajumuisha miezi 30 ambapo atakaa chini ya uangalizi na kutozwa faini ya dola 145,000 (£110,000) sawa na Tsh 335,766,491. Kesi hiyo ilitokana na tukio la miaka mitatu iliyopita ambapo Smollett alisema alishambuliwa na watu wawili.