Hatimaye muigizaji maarufu kutoka nchini Marekani, Julia Fox ameamua kuingilia kati tetesi zinazoenea kwa kasi mitandao kuhusu mahusiano yake na rapa Dizzy Drake, zilizovuma punde baada ya mrembo huyo kuingia kwenye uhusiano wa kimapenzi na Rapa Kanye West ambaye hivi karibuni alimaliza bifu lake na Drake.
Julia ameweka wazi kutofurahishwa na kitendo cha watu kueneza taarifa hizo licha ya kuwa hazina ukweli wowote ndani yake kwa madai ya kuwa Drake alikuwa rafiki yake wa kawaida na hawakuwahi kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi kabisa.
"Drake ni mtu mzuri na muungwana, Hakuna chochote kilichotokea kati yetu, tulikuwa pamoja kama marafiki wa kawaida tukibarizi." Alisema Julia Fox