Msanii wa Filamu Bongo, Johari amedai iwapo ikatokea Gabo na Ray Kigosi wakamtongoza atahisi wamechangany
Muigizaji amesema Gabo na Ray ni kama kaka zake na yeye ni dada kwao, hivyo wakidhubutu kufanya hivyo atapeleka hospitali kwani watakuwa wamechanganyikiwa.
“Kwanza (Gabo) hatoweza kunitongoza kwa sababu mimi na yeye ni kama dada na kaka, tunaheshimina na ni ndugu, sasa atanitongozaje,” ameeleza.
Johari amesema hayo kupitia Kikaangoni, EATV, alipoulizwa kuhusu Ray Kigosi alijibu; “Nitamkatalia, mimi nitamkatalia!, sasa unajuaje mimi ni mtalaka wake?, hamna hawawezi, mimi nitawapeleka hospitali nitajua wamechanganyikiwa”.