Rapa wa muziki wa Bongo Fleva kutoka kundi la Weusi ambaye amewahi kufanya kazi na AKA, Don't Bother, Joh Makini amefunguka kwa urefu na kutoa pole kwa familia ya AKA pia namna alivyofanikisha collabo yao.
Joh Makini ameeleza kusikitishwa na taarifa hizo huku akisema atamiss ukarimu wa AKA kwa kuwa alikuwa mtu poa sana, Joh Makini amefunguma kuwa hakutegemea kama AKA angekuwa mtu mkarimu sana kwa alivokuwa akimuona kabla ya kukutana Dar es Salaam.
Ameongeza kuwa kitu ambacho hawezi kukisahau ni namna collabo yao ilivyofanikiwa nna hata siku wanaingia studio AKA alianza kurekodi na Diamond Platnumz ngoma yao ya MAKE ME SING lakini aliomba Joh Makini asubiri mpaka pale atakapomaliza.