Baada ya kutemana na ‘lebo’ yake ya ‘emPawa’ mwanamuziki kutoka nchini Nigeria Joe boy ameripotiwa kujiunga na ‘Warner Music’, akiungana na ma-staa kama #Diamond, Burna Boy, Ed Sheeran, Cardi B na wengineo.
Licha ya kujiunga na ‘lebo’ hiyo kubwa Joeboy pia amezindua record Labe yake aliyoipa jina la ‘Young Legend labe’.
Akiwa chini ya ‘emPawa’ Joeboy amewahi kuachia album mbili, na Ep mbili zikiwemo Magic And Body Soul na Somewhere Between Beauty, pia aliweza kuachia ngoma kama ‘All For You’, ‘Lonely’, pia amewahi kushirikishwa kwenye ‘kolabo’ na mwanamuziki #Zuchu katika wimbo wa ‘Nobody’.