Menu ›
Burudani
Tue, 7 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rapa mkongwe Bongo, Hery Samir maarufu kama Mr Blue Byser amesema kuwa jina lake jipya anaenda kama "King Wa Rap".
"Jina langu jipya naitwa King Wa Rap, Mungu wangu aliye juu hawezi kukubali unishushe chini" - ameandika Mr Blue
Mr Blue amejipa jina hilo baada ya wasanii wengi kama Madee, Q Chief, Babalevo, P Mawenge, Conboi, Young Dee, Nyandu Tozzy na Sholo Mwamba kuukubali uwezo wake wa kimuziki na ustaa mkubwa alionao.
Baadhi ya majina mengine ambayo anatambulika nayo Mr Blue ni Kherry Samir, Byser Babilone, Nyani Zee na hili jipya la King Wa Rap.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live