Menu ›
Burudani
Sat, 18 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Dada mkubwa, Judith Wambura 'Lady Jaydee' usiku wa kuamkia leo Novemba 18, 2023 amefanya bonge shoo katika usiku wake alioupa jina la Statement pale Nyumbani Lounge.
Pamoja na kuwa na mvua kali na eneo kubwa kuwa wazi, mashabiki hawakusita kuimba naye mwanzo mwisho hususan wimbo wa Mambo Matano ambao ndio habari ya mjini kwa sasa.
Mbali na kuimba naye, mashabiki hao 'waliochizika' kwa shoo, walimfuata kwenye jukwaa na kumtunza pesa huku wakiendelea kucheza.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live