Ni Headlines za mwanamuziki tajiri duniani #JayZ ‘HOV’ akiwachana waandaji wa tuzo za Grammy kutompa tuzo yoyote mke wake @Beyonce kipengele cha Album bora ya mwaka.
Jay Z amefunguka hilo wakati anapokea tuzo ya ‘Dr Dre Global Impact Award’ akihoji kwanini Beyonce ana tuzo nyingi za Grammy kuliko mtu yeyote na nyimbo zake kutoka kwenye Album ndio zinachukua lakini hapewi tuzo ya Album bora ya mwaka.
“Inakuaje ana tuzo nyingi za Grammy kuliko mtu yeyote, halafu unakosa tuzo ya Album bora ya mwaka? Hiyo haifanyi kazi fikirieni kuhusu hilo, wengi wataenda nyumbani kuhisi kama ameibiwa,” amesema Jay Z.