Jarida maarufu la mitindo nchini Marekani la Vanity Fair limeshambuliwa vikali na wapenzi wa mitindo duniani baada ya kuchapisha picha ya juu ya jarida hilo likimuonesha mwanamama Oprah Winfrey akiwa na mikono mitatu.
Jarida hilo ambalo linatoka mara moja kwa mwaka halikukosea kwa mtu mmoja kwani picha nyingine ya Muigizaji Reese Witherspoon ambaye na yeye ameonekana na miguu mitatu kwenye picha hiyo ya mbele.
Baada ya cover hilo lililokosewa kuchapishwa mtandaoni usiku wa kuamkia leo mashabiki wamelishambulia wakidai kuwa kwanini waandaaji hawakutumia picha za asili bila kuzihariri (Editing).
Photoshop fail gave Oprah Winfrey three hands and Reese Witherspoon three legs in Vanity Fair.