Jane Fonda (85) mwigizaji maarufu Marekani ambaye yupo singo, katika mahojiano mapya alipoulizwa kuhusu kuwa katika mahusiano katika umri alionao sasa.
Amejibu kwa kusema anajisikia aibu kwa anachoongea ila kama ni lazima awe katika mahusiano katika umri alionao, atachagua mwanaume mwenye miaka 20 ndie awe mpenzi wake.
Alipoulizwa kwa nini mwanaume mwenye miaka 20, amejibu kwa sababu hapendi ngozi kongwe zilizozeeka, ambapo aliibua vicheko kwa mtangazaji na producers wa kipindi ingawa Jane yeye alibaki kuwa serious.
Jane ambaye alishaingia kwenye ndoa tatu na kujaaliwa watoto watatu wenye miaka 55, 54 na 49, hata hivyo kwa muda mrefu ameamua kuwa single akionekana hana nia tena ya kuwa katika mahusiano tofauti na mitazamo ya wengi kuwa uzeeke ukiwa na mwenza.