Menu ›
Burudani
Thu, 23 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwanamke mmoja ambaye jina lake halijafahamika, amemfungulia mashtaka Mwigizaji Jamie Foxx akimtuhumu kwa kutaka kumbaka na kumfanyia vitendo vya unyanyasaji wa kingono.
Kwa mujibu wa TMZ ambao wamelinasa shauri hilo, mwanamke huyo alikutana na Foxx mjini New York mwaka 2015.
Baada ya kumtambua kuwa ni Jamie Foxx, mwanamke huyo aliomba kupiga naye picha.
Punde baada ya kumaliza tu, mambo yalianza kwenda tofauti ambapo mwanamke huyo anadai Foxx alianza kumshika kifuani na sehemu za siri bila ridhaa yake huku akimtamkia maneno ya mahaba.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live