Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ishu ya umri ya Wema Sepetu kumfikisha hapa, Basata wafunguka

Wemaaaaaa+pic Ishu ya umri ya Wema Sepetu kumfikisha hapa, Basata wafunguka

Wed, 30 Sep 2020 Chanzo: mwanaspoti.co.tz

HUKO kwenye mitandao ya kijamii habari ya mjini ni ‘birthday’ ya mrembo wa Tanzania wa mwaka 2006, Wema Sepetu ambaye kila Septemba 28 anasherehekea siku yake ya kuzaliwa.

Juzi mrembo huyo aliposti kwenye mtandao wa kijamii akisherehekea siku yake ya kuzaliwa na kueleza kutimiza miaka 30 jambo lililoibua mjadala mzito.

Hata hivyo, hesabu za umri huo na mwaka alioshiriki na kushinda taji la Miss Tanzania viligonga vichwa vya watu, kwani moja ya masharti ya kushiriki shindano hilo ni lazima mhusika atimize miaka 18 hadi 23, hivyo kama Wema alidanganya, alishinda taji hilo akiwa na miaka 16.

Wafuasi wake mitandaoni walimbana kwa maswali kuhusu umri wake na kwa mara ya kwanza juzi akakiri, ndio ametimiza miaka 30.

Mwenyewe akafunguka laivu, amezaliwa mwaka 1990 na wakati anashinda taji la Miss Tanzania alikuwa na miaka 16. Akadai alidanganya umri ili kupata fursa ya kushiriki shindano hilo ambalo Jokate Mwegelo alishika namba mbili. Kitendo cha Wema kukiri kudanganya kisheria ni kosa na kwa mujibu wa wakili Kasanda Mitungo, moja ya adhabu za kudanganya umri na kama itathibitika ni kuvuliwa taji hilo.

Ingawa Kasanda amebainisha, kuvuliwa taji hilo pia kutategemea na kanuni za shindano ingawa kikanuni, mshiriki hapaswi kuwa na miaka chini ya 18 au zaidi ya 23.

Chanzo: mwanaspoti.co.tz