Dar es Salaam. Msanii wa filamu nchini Tanzania, Irene Uwoya amewaomba radhi waandishi wa habari kutokana na kitendo chake cha kuwarushia fedha katika mkutano.
Uwoya ametoa kauli hiyo leo Jumatano Julai 17, 2019 baada ya kumalizika kwa kikao kati yake na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) ambacho pia kilimhusisha msanii mwenzake, Steve Nyerere.
Wawili hao waliitwa na Basata jana baada ya Uwoya kutumia mkutano wa wasanii na waandishi wa habari kuwarushia fedha jambo lililozua mjadala ikiwamo kuonyesha dharau kwa wana taaluma hao.
“Mimi binafsi naomba samahani lakini sikufanya makusudi kama watu walivyotafsiri, nilifanya hivyo kwa furaha zangu tu kwa kuwa mlikuja kwa wingi,” amesema Uwoya.
Amebainisha kuwa hakukuwa na mpango wa kuwadhalilisha waandishi wa habari, na kwamba alilenga kuwatunza lakini ametafsiriwa vibaya.
Leo wawili hao walifika Basata kuitikia wito wa baraza hilo. Walifika saa 4:30 na gari aina ya Toyota Prado nyeusi.
Pia Soma
- Sababu Mtwara kuporomoka mikoa iliyofanya vyema kidato cha sita hii hapa
- Steve Nyerere, Irene Uwoya hawajasajiliwa Basata
- Uchaguzi serikali za mitaa, Lugola avionya vyama vya siasa Tanzania
Ilipofika saa 4:45 asubuhi wasanii hao walishuka kwenye gari hilo na kuelekea ndani ya ofisi ya Katibu Mtendaji wa Basata.