Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ilifika hatua msanii akiambiwa katekwa anaona ndio kiki – Nikki Mbishi

3653 28157115 165344494113845 8688680786397757440 N TZW

Mon, 26 Feb 2018 Chanzo: bongo5.com

Msanii wa muziki wa hip hop Bongo, Nikki Mbishi amesema katika muziki huo  kuna wasanii wanaendekeza sana kiki kuliko muziki wao.



Rapper huyo ameiambia The Playlist ya Times Fm kuwa kitendo hicho is kizuri katika muziki na amekuwa akikemea katika ngoma zake.

“Kuna wakati ulifikia sijui bado upo au unaendelea matukio ya kisiasa yalikuwa yanafunika hata muziki mtu unatoa ngoma yako watu wanataka kusikia mambo yako mengine,” amesema Nikki Mbishi.

“Ilifika hatua hiyo wasanii wengi wakawa mtu akiambia katekwa anaona ndio kiki, inaonekana ndio dili, kwa hiyo kila mtu ndio anajifanya kama kapotea, katekwa mara sijui kahusishwa na vitu gani na serikali ilimradi iwe hivyo,” ameongeza.

Nikki Mbishi kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la Nimekumiss.

Chanzo: bongo5.com