Menu ›
Burudani
Wed, 11 Aug 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchekeshaji na Muigizaji Idris Sultan ndiye Mtanzania pekee ambaye ametokea kwenye orodha ya mastaa wa dunia ambao wametengeneza pesa ndefu kupitia mtandao wa instagram mwaka 2021 (Instagram Rich List), kwa mujibu wa tovuti ya HopperHQ.
Idris Sultan mwenye jumla ya wafuasi 7M kwenye akaunti yake ya Instagram yupo kwenye nafasi ya 108, akitajwa kutoza kiasi cha ($42,800) TZS. Milioni 99.2 Ku-post Tangazo la Biashara.
Mitandao ya Kijamii ni moja ya "Platform" nzuri ambazo mtu mwenye wafuasi wengi anaweza kuzitumia na kuingiza kipato kikubwa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live