Msanii kutoka Lebo ya Konde Music, @ibraah_tz amefunguka kuhusu ushindani kwenye game kwa upande wako hana kabisa kwasababu anafanya muziki wake peke yake na wengine wanafanya muziki wao peke yao.
"Sioni kama kuna ushindani wowote kwasababu #ibraah ni #ibraah na msanii mwingine ni msanii mwingine, sishinidani na mtu nafanya muziki wangu na mimi ni mfalme wa new school (kizazi kipya) na sidhani kama kuna king nimemkuta hivyo mimi ndio king.
“Kunishindanisha na kina #dayoo nikunirudisha nyuma kwasababu wasanii tuliotoka pamoja tulikuwa wachache tu na sidhani kama ukimsimamisha kwenye matukio ambayo nimekutana nayo mimi atasurvive," amesema Ibrah.