Ni 'headlines' za msanii Ibraah kutoka Konde Music Wordwide ambaye amekana kuwa kwenye penzi na msanii wa filamu na video vixen Nanah aliyechora tattoo yenye jina lake shingoni.
Submitted by Shaluwa Anta on Jumatatu , 3rd Mei , 2021 Kushoto ni msanii Ibraah na mrembo Nanah, kulia ni tattoo aliyochorwa Ibraah
Akizungumzia hilo kupitia Kamera ya EATV & EA Radio Digital, Ibraah amesema kuchorwa tattoo na mrembo huyo haihusiani kwamba ndio wapo kwenye mahusiano bali kilichokuwepo kwao ni upendo na urafiki.
"Nanah sio mtu wangu ni rafiki yangu na ana mahusiano yake, kuhusu tattoo kila mtu anaamua kuchora, nilivyomuona nilimuuliza akasema amependa tu kuchora jina la Ibraah kwa sababu mimi ni mtu wake wa karibu na nina umuhimu kwake, mbona kuna watu wengi wamenichora ila wanamsema Nanah tu" amesema IbraahÂ
Pia ameendelea kusema urafiki wao kwa sasa una muda wa miezi 6 na kinachoendelea kati yao ni upendo tu.